KUZALIWA KWAKE.
Diamond alizaliwa tarehe 2, October mwaka 1989 katika Hospitali
ya Amana Dar es salaam na kupewa jina la
Nasibu Abdul Juma . Akiwa na umri mdogo wazazi wake walitengana na
baba yake kumuacha bila msaada wowote na ikabidi wahamie Tandale
Magharibi kwa bibi yake mzaa mama, na hapo ndipo yakawa makazi yao..
Historia yake ni ya kusikitisha kama alivyoelezea kwenye wimbo wa binadamu
wabaya.
ELIMU YAKE.
Mnamo mwaka 1995 alianza kupata elimu ya Nursery katika
shule ya Chakula Bora iliyopo Tandale Uzuri hadi alipomaliza na kujiunga
na Elimu ya Msingi yaani (Primary School) mwaka 1996 katika shule ya
msingi Tandale magharibi iliyopo jijin Dar-es-salaam na kuhitimu shule ya
Msingi mwaka 2002. Baadae akahitimu elimu yake ya Secondary mwaka 2006.
SAFARI YAKE YA MUSIKI NA
MAFANIKIO YAKE.
Akiwa darasa la tano diamond alionekana kuanza kupenda
sana muziki, hivyo alianza kunakili baadhi ya nyimbo na
kukariri nyimbo za wasanii waliokuwa makihri ndani na nje ya nchi
kwa kipindi hicho na kuwa anaimba katika sehemu tofautitofauti.Mara nyingi
mama yake alikuwa akimnunulia kanda za album za wasanii tofauti
waliokuwa makihiri kipindi hicho na hata kumuandikia baadhi ya nyimbo za
wasanii hao ili mwanae aweze kuzishika na kuimba kirahisi, na wakati
mwingine hata kumpeleka katika matamasha tofautitofauti ya vipaji vya
watoto ili mwanae apate nafasi ya kuimba, kitu ambacho baadhi ya ndugu wa
familia waliona ni kama kumpotosha na kumuharibu mtoto huyo badala ya
kumuhimiza kimasomo. Kiukweli hali ya maisha yao ilikuwa ni ngumu
saana, maana mama Diamond hakuwa hana mradi wowote ya kumuingizia kipato,
hivyo ilibidi atumie kias kidogo anachokipata toka kwa kodi ya vyumba
viwili alivyopewa na Mama yake yaani bibi yake diamond na vibiashara vyake
vidogovidogo vya mikopo kwa kumsomeshea na kumlea diamond. Hali yao
ya Kimaisha ilikuwa ni ngumu sana, hivyo iliwaradhimu wote kuhamia katika
chumba cha bibi huyo ili kupangisha vyumba vile viwili alivyopewa
mama diamond
mama diamond
Ilipofika mwaka 2003 baada ya Diamond kutaka kuanza masomo ya Secondary mama yake alimwambia aachane na muziki
kabisa na azingatie na Masomo ili aweze kupata elimu itayomsaidia hata kwa
muziki wake baadae kwa maana asingeweza kushika vitu viwili kwa pamoja
muda huo. Akiwa secondary diamond aliendelea kufanya muziki kisirisiri
bila mama yake kujua na kufikia mwaka 2004 taratibu akaanza kujifunza
kuandika nyimbo zake mwenyewe. 2006 mwaka 2007 alijikita rasmi katkia sughuri
za muziki ili kujaribu kutimiza ndoto zake.kiukweli haikuwa ni safari
rahisi kama alivyotegemea hadi kupelekea mda kuanza kutafuta vibarua
toafauti tofauti ili mradi aweze kupata riziki na kuepuka hali ya
kushinda nyumbani, ikiwemo kuuza mitumba, petrol station, kupiga
picha,kazi za viwandani hata wakati mwingine kuingia kwenye makundi ya
kucheza kamali za mitaani ili aweze kupata pesa ya kuingia studio
kurecord lakini bila kufanikiwa, kiukweli ikabidi imradhimu kuuza pete ya
Dhahabu ambayo alipewa na mama yake mzazi aivae na kumdanganya kuwa
ameipoteza na ndipo hapo alipofanikiwa kuingia studio kurecord nyimbo ya
kwanza iitwayo ‘TOKA MWANZO’
kutokana na kutokuwa na mazoea ya kurecord hakuweza kutengeneza nyimbo
ambayo ilivuma sana lakini wimbo ule ulianza kumpa jina kutokana na watu
wengi walishangazwa jinsi alivyoingia kwa mara ya kwanza studio na kuweza
kutengeneza wimbo kama mtu ambae ni mzoefu, hivyo iliwafanya kuamini
kuwa akipata nafasi ya kurecord mara kadhaa angeweza kufanya kitu
kikubwa..Wimbo ule ulimfanya aweze kukutana na Chizo mapene ambae alijitolea kumsimamia kazi zake na
wakaanza kurecord album lakini bahati mbaya wakiwa katikati ya kurekodi album
hiyo anayemsaidia alipata matatizo ya kifedha na hakuweza tena kumsaidia
hivyo ilimbidi Diamond aanze tena upya kuzunguka katika studio tofauti
kuomba kuingia mkataba kwenye record label lakini kote hakuweza kufanikiwa,
wote walimwambia bado hajui kuimba na kutotaka kumsikiliza kabisa.Kilikuwa ni
kipindi kigumu sana maana hata yule mpenzi wake ambae alikuwa nae alimuacha
kwakua alikuwa ameshachoshwa na ndoto hewa ambazo alikuwa akiziota kila
siku diamond kuwa ipo siku atafanikiwa kimuziki na kuwa mwanamuziki mkubwa na
wao kuish maisha
mazuri, kitu ambacho kilimchanganya na kumuumiza sana Diamond.Mwaka
2009, Diamond alikutana na Bwana Msafiri
Peter maarufu kama Papaa
Misifa ambae alikubali kumsaidia kimuziki na kurecord wimbo wa kwanza ulioenda
kwa jina la “KAMWAMBIE”, ni wimbo
ambao Diamond aliimba kwa uchungu huku akimuimbia mpenzi wake
huyo aliyemuacha (Sarah Sadiki)
kuelezea kiasi gani aliumia kwa yeye kumuacha kwake, na hapo ndipo
taratiibu nyota yake
ikaanza kung’aa na wimbo huo kukua siku hadi siku.Maisha yake yakabadilika na Diamond kuweza kununua gari aina ya Toyota Celica. Tarehe 14/02/2010 Diamond aliachia album yake ya kwanza iliyokuwa na nyimbo 10 ambazo ni kamwambie , Mbagala , Nitarejea , Nalia na mengi , Binadamu , Nakupa , Usisahau , Uko tayari , Wakunesanesa , Toka mwanzo na Jisachi. Mnamo tarehe 04 mwezi wa 4 mwaka 2010 , Diamond aliandika record ya kuwa msanii wa kwanza Tanzania kushinda tunzo tatu za Tanzania Kili Music Awards kwa pamoja
ambazo ni: Msanii bora Chipukizi, Wimbo bora wa Mwaka (KAMWAMBIE) na Wimbo bora wa R&B(KAMWAMBIE), tunzo ambazo zilimfanya achaguliwe kuwa balozi wa Malaria nchini Tanzania.Baada ya kuachia wimbo wake wa pili unaoitwa Mbagala, Diamond alichaguliwa na Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Dr Jakaya Mrisho kikwete kuwa mtumbuizaji katika safari nzima ya Kampeni yake. Tarehe 02 -10 -2010 alipa safari ya kwanza kwenda England mjini LONDON,MILTON KEYNES, na COVENTRY. Baada ya kuachia wimbo wake wa tatu mwaka 2011 , Diamond alishinda tuzo ya
Nzumari Award nchini Kenya akiwa kama Msanii bora wa Kiume toka Tanzania. Diamond aliachia nyimbo yake ya nne na kuweka record ya kuwa msanii wa kwanza na pekee kujaza Club Maisha hadi watu kushindwa kuingia na hata wengine kuzimia baada kutokupata hewa ya kutosha kutokna na wingi ujaaji huo.Mwaka mpya wa 2012, tarehe 1 -1- 2012 , Diamond Platnumz aliachia album yake ya pili na kuweka record ya kuwa msanii wa kwanza Tanzania kuuza zaidi ya nakala 1200,000 . Mwanzoni mwa mwaka 2012 Diamond aliweka record kuwa msanii wa kwanza Tanzania kufanya show ya USHIRIKIANO iliyoitwa ” Diamond forever” iliyofanyika Mlimani City kwa kiinglio cha shilingi elf hamsini 50,000 za kitanzania akiwa pekeake na kuuza ticket zaidi ya 1,500.Mnamo mwezi wa 5 mwaka 2012 , Diamond Platnumz aliweka record ya kuwa msanii wa kwanza kufanya show na kujaza zaidi ya watu 10’000 kwa kiingilio cha 20,000 katika kiwanja cha Darlive huku akishuka na Helicopter kwenye Stage. Mwaka huohuo Diamond alifanya ziara yake ya Europe ikiwemo Italy, Holland, Sweden , Greece na kumalizia ziara yake ya arabuni nchini Masqat Oman.Mwishoni mwa mwaka 2012 ulikua mzuri kwa Diamond Platnumz kwani aliweza kuachia nyimbo mbili kwa mpigo za “Nataka kulewa ” na “Kesho ”.Mwezi wa kumi na mbili mwaka 2012 diamond alitajwa kuwa ni msanii wa kwanza anaelipwa Pesa nyingi kwenye Show toka Tanzania Mwanzoni mwa mwaka 2013 , Diamond Platnumz alichaguliwa na Cocacola kuwa Balozi wa Kinywaji Cha Cocacola, na kufuatiwa na ziara yake ya East Africa na ikiwemo Burundi , Congo na Kenya n.k. na kuweka record ya kuwa msanii wa kwanza East Africa kuwezakupiga show pekeake kwenye uwanja na kujaza zaidi ya watu 30,000… mnamo June 2013 Diamond alishinda tuzo mbili za Tanzania Kili Music Award akiwa kama Msanii bora wa kiume Bongoflavour na Msanii bora wa kiume kwa wanamziki wote Tanzania.Mwezi wa saba mwaka 2013 , Diamond aliachia nyimbo yake yake iliyokwenda kwa jina la Number One ambayo aliifanyia Video Capetown South Africa chini ya kampuni ya Ogopa Videos na kuweka record ya kuwa msanii wa kwanza kulaunch video bila kiingilio katika Hotel ya SERENA na kuwaalika, na viongozi toka sehemu tofauti tofauti. katika chakula cha mchana hiyo akamzawadia Gari moja ya nguri mkubwa katika mziki wa Tanzania , Marehemu Mwidini Gurumo.mwezi 10 mwaka 2013 .Diamond aliifanya Collabo na msanii toka Nigeria Davido katika wimbo wake wa Number one kama Remix kutoa video ya wimbo huo na Kampuni ya Capital Dreams iliyo chini ya Director Clarence Peter. Nyimbo hii ilimtambulisha Diamond Platnumz nchini Nigeria na barani Africa kiujumla na kumuwezesha kupata nominations mbalimbali kwenye tuzo za kimataifa ikiwemo , MTV MAMA awards ambayo aliperform nyimbo hii live na Davido, BET Awards na tuzo zinazotegemea kufanyika za AFRIMAMA , MTV Europe , Channel O awards na awards nyingine kutoka nchi mbalimbali.Tarehe 7 - 7 - 2014 , wakati Diamond akisherekea Birthday ya mama yake alimzawadia mama yake gari pamoja na kuachia video mbili za mdogomdogo aliyoifanyia nchini Uingereza na BumBum aliyomshirikisha Iyanya kutoka Nigeria aliifanyia Afrika Kusini. Video hizi kwa pamoja zilimgarimu Diamond dola 78,000 za kimarekani . Hivi Sasa nyimbo hizi ndio habari ya mjini na ni kitu kisichofikisha kwamba nyimbo hizi zitaendelea kumbeba Diamond hadi mwaka 2014 unaisha.Huyu ndio Diamond Platnumz, mtoto wa Tandale aliyoweza kutumia kipaji chake cha kuimba vizuri, aliyoweza kukabiliana na changamoto mbalimbali za maisha ,maisha yake ni fundisho kwa vijana kibao mjini wanaohangaika kutoka kimaisha.
ikaanza kung’aa na wimbo huo kukua siku hadi siku.Maisha yake yakabadilika na Diamond kuweza kununua gari aina ya Toyota Celica. Tarehe 14/02/2010 Diamond aliachia album yake ya kwanza iliyokuwa na nyimbo 10 ambazo ni kamwambie , Mbagala , Nitarejea , Nalia na mengi , Binadamu , Nakupa , Usisahau , Uko tayari , Wakunesanesa , Toka mwanzo na Jisachi. Mnamo tarehe 04 mwezi wa 4 mwaka 2010 , Diamond aliandika record ya kuwa msanii wa kwanza Tanzania kushinda tunzo tatu za Tanzania Kili Music Awards kwa pamoja
ambazo ni: Msanii bora Chipukizi, Wimbo bora wa Mwaka (KAMWAMBIE) na Wimbo bora wa R&B(KAMWAMBIE), tunzo ambazo zilimfanya achaguliwe kuwa balozi wa Malaria nchini Tanzania.Baada ya kuachia wimbo wake wa pili unaoitwa Mbagala, Diamond alichaguliwa na Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Dr Jakaya Mrisho kikwete kuwa mtumbuizaji katika safari nzima ya Kampeni yake. Tarehe 02 -10 -2010 alipa safari ya kwanza kwenda England mjini LONDON,MILTON KEYNES, na COVENTRY. Baada ya kuachia wimbo wake wa tatu mwaka 2011 , Diamond alishinda tuzo ya
Nzumari Award nchini Kenya akiwa kama Msanii bora wa Kiume toka Tanzania. Diamond aliachia nyimbo yake ya nne na kuweka record ya kuwa msanii wa kwanza na pekee kujaza Club Maisha hadi watu kushindwa kuingia na hata wengine kuzimia baada kutokupata hewa ya kutosha kutokna na wingi ujaaji huo.Mwaka mpya wa 2012, tarehe 1 -1- 2012 , Diamond Platnumz aliachia album yake ya pili na kuweka record ya kuwa msanii wa kwanza Tanzania kuuza zaidi ya nakala 1200,000 . Mwanzoni mwa mwaka 2012 Diamond aliweka record kuwa msanii wa kwanza Tanzania kufanya show ya USHIRIKIANO iliyoitwa ” Diamond forever” iliyofanyika Mlimani City kwa kiinglio cha shilingi elf hamsini 50,000 za kitanzania akiwa pekeake na kuuza ticket zaidi ya 1,500.Mnamo mwezi wa 5 mwaka 2012 , Diamond Platnumz aliweka record ya kuwa msanii wa kwanza kufanya show na kujaza zaidi ya watu 10’000 kwa kiingilio cha 20,000 katika kiwanja cha Darlive huku akishuka na Helicopter kwenye Stage. Mwaka huohuo Diamond alifanya ziara yake ya Europe ikiwemo Italy, Holland, Sweden , Greece na kumalizia ziara yake ya arabuni nchini Masqat Oman.Mwishoni mwa mwaka 2012 ulikua mzuri kwa Diamond Platnumz kwani aliweza kuachia nyimbo mbili kwa mpigo za “Nataka kulewa ” na “Kesho ”.Mwezi wa kumi na mbili mwaka 2012 diamond alitajwa kuwa ni msanii wa kwanza anaelipwa Pesa nyingi kwenye Show toka Tanzania Mwanzoni mwa mwaka 2013 , Diamond Platnumz alichaguliwa na Cocacola kuwa Balozi wa Kinywaji Cha Cocacola, na kufuatiwa na ziara yake ya East Africa na ikiwemo Burundi , Congo na Kenya n.k. na kuweka record ya kuwa msanii wa kwanza East Africa kuwezakupiga show pekeake kwenye uwanja na kujaza zaidi ya watu 30,000… mnamo June 2013 Diamond alishinda tuzo mbili za Tanzania Kili Music Award akiwa kama Msanii bora wa kiume Bongoflavour na Msanii bora wa kiume kwa wanamziki wote Tanzania.Mwezi wa saba mwaka 2013 , Diamond aliachia nyimbo yake yake iliyokwenda kwa jina la Number One ambayo aliifanyia Video Capetown South Africa chini ya kampuni ya Ogopa Videos na kuweka record ya kuwa msanii wa kwanza kulaunch video bila kiingilio katika Hotel ya SERENA na kuwaalika, na viongozi toka sehemu tofauti tofauti. katika chakula cha mchana hiyo akamzawadia Gari moja ya nguri mkubwa katika mziki wa Tanzania , Marehemu Mwidini Gurumo.mwezi 10 mwaka 2013 .Diamond aliifanya Collabo na msanii toka Nigeria Davido katika wimbo wake wa Number one kama Remix kutoa video ya wimbo huo na Kampuni ya Capital Dreams iliyo chini ya Director Clarence Peter. Nyimbo hii ilimtambulisha Diamond Platnumz nchini Nigeria na barani Africa kiujumla na kumuwezesha kupata nominations mbalimbali kwenye tuzo za kimataifa ikiwemo , MTV MAMA awards ambayo aliperform nyimbo hii live na Davido, BET Awards na tuzo zinazotegemea kufanyika za AFRIMAMA , MTV Europe , Channel O awards na awards nyingine kutoka nchi mbalimbali.Tarehe 7 - 7 - 2014 , wakati Diamond akisherekea Birthday ya mama yake alimzawadia mama yake gari pamoja na kuachia video mbili za mdogomdogo aliyoifanyia nchini Uingereza na BumBum aliyomshirikisha Iyanya kutoka Nigeria aliifanyia Afrika Kusini. Video hizi kwa pamoja zilimgarimu Diamond dola 78,000 za kimarekani . Hivi Sasa nyimbo hizi ndio habari ya mjini na ni kitu kisichofikisha kwamba nyimbo hizi zitaendelea kumbeba Diamond hadi mwaka 2014 unaisha.Huyu ndio Diamond Platnumz, mtoto wa Tandale aliyoweza kutumia kipaji chake cha kuimba vizuri, aliyoweza kukabiliana na changamoto mbalimbali za maisha ,maisha yake ni fundisho kwa vijana kibao mjini wanaohangaika kutoka kimaisha.
The article is really good, permission to comment here admin Pesona mata
ReplyDelete